Sep 19, 2012

MABADILIKO YA JINA KWA BLOG HII

SASA
  STUDIO FIVE NEWS.BLOGSPORT.COM
INAITWA   
BLOGTZ.BLOGSPORT.COM


TANGU SEPT 12. 2012

Tupate: www.blotz.blogsport.com


Sep 12, 2012

RAIS KIKWETE AFANYA ZIARA RASMI YA KISERIKALI YA SIKU TATU NCHINI KENYA

Mhe. Rais Jakaya Kikwete na ujumbe wake ktoka Tanzania wakiwasili na kulakiwa na mwenyeji wao Mhe.Mwai E. Kibaki katika Ikulu ya Nairobi nchini Kenya Sept.11.2012.
Rais Kikwete na ujumbe wake wako katika  ziara ya kiserikali kwa siku tatu nchini humo.

 Rais Jakaya Kikwete akikata utepe kufungua rasmi jengo la Shule ya Ukarimu na Utalii ya Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya. Kulia kwake ni Waziri wa Elimi ya Juu nchini Kenya, na kushoto kwake ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kenyatta ,Profesa Olive Mugendi.

 Rais Jakaya Kikwete akihutubia hadhara na kufungua rasmi jengo la Shule ya Ukarimu na Utalii ya Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya.

Waheshimiwa Marais Jakaya Kikwete na mwenyeji wake Mwai E. Kibaki pamoja na wajumbe kutoka nchi zote mbili(Tanzania na Kenya) wakiwa katika picha ya pamoja nje ya jengo la Ikulu,Jijini Nairobi

BREAKING NEWS..............................

Askari polisi anayetuhumuwa kumuua mwandishi wa habari marehemu Daudi Mwangosi afikishwa rasmi leo katika Mahakama ya Hakimu mkazi Mjini Iringa akikabiliwa na shitaka la kuua kwa kukusudia. Kesi hiyo inasikilizwa na Mhe.Hakimu Dyness Lyimo.
Mtuhumiwa alitajwa kwa jina la Pc Pafificius Cleophace Simon mwenye No.2573, umri miaka 23.
Hata hivyo kutokana na uzito wa shitaka lake, afande huyo hakupaswa kujibu chochote na kesi yake imaehirishwa hadi tarehe 26 Sept. 2012 . 
Globu hii ya kijamii itaendelea kukuhabarisha currently